John 21:1-6

Isa Awatokea Wanafunzi Saba

1 aBaada ya haya Isa akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia.
Yaani Bahari ya Galilaya.
Yeye alijionyesha kwao hivi:
2 cSimoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja. 3 dSimoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.

4 eMara baada ya kupambazuka, Isa akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Isa.

5 fIsa akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?”

Wakamjibu, “La.”

6 gAkawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.

Copyright information for SwhKC